π Historia ya Afisi ya Mwanasheria Mkuu
Safari ya kihistoria tangu enzi za ukoloni hadi leo
Kabla ya Mapinduzi ya 1964
Afisi ya Mwanasheria Mkuu ni kati ya taasisi kongwe iliyoanzishwa na wakoloni mnamo mwaka 1913β1914. Kazi yake kuu ilikuwa kutoa ushauri kwa Serikali na kusimamia masuala yote ya kisheria kwa niaba ya Serikali.
Mwaka 1926 Mwanasheria Mkuu alikua miongoni mwa wajumbe wa Baraza la Kutunga Sheria na Utawala, akiendelea hadi mwaka 1936, wakati Baraza lilipoendelea hadi Mapinduzi ya mwaka 1964.
Baada ya Mapinduzi ya 1964
Baada ya Mapinduzi, Afisi ya Mwanasheria Mkuu iliendelea kutekeleza majukumu ya kisheria ikiwemo usimamizi wa kesi za jinai. Nafasi hii ilitambuliwa rasmi na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 chini ya kifungu cha 55(1).
Kwa sasa, kazi na majukumu yameongezeka kwa mujibu wa Sheria ya Afisi ya Mwanasheria Mkuu (Utekelezaji wa Majukumu) Nam. 6 ya 2013, sambamba na maendeleo ya kiuchumi na kisiasa.
π Faili la PDF linajumuisha historia kamili ya Afisi ya Mwanasheria Mkuu