Usimamizi wa Kesi za Madai
Huduma kutoka Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar
Muhtasari wa Huduma
Afisi ya Mwanasheria Mkuu inatoa huduma ya kuiwakilisha Serikali katika kesi na mashauri ya madai. Pia inashiriki katika usuluhishi, upatanishi na utatuzi wa migogoro ikiwa Serikali ni sehemu ya kadhia hiyo.
Majukumu Makuu
Kusimamia kesi na mashauri ya madai yaliyofunguliwa na Serikali au dhidi ya Serikali.
Kutoa miongozo juu ya usimamizi wa kesi na kuhakikisha utekelezaji wake.
Kutoa maelekezo yanayohusiana na usimamizi wa kesi.
Kufungua kesi ya madai dhidi ya Afisa wa Serikali aliyeshughulikia vibaya kesi (Sheria No. 3 ya 2010).
Kufanya mashauriano na taasisi binafsi au za Serikali kutatua migogoro nje ya Mahakama.
Kutoa ushauri wa kisheria kwa Serikali.